• Sera yetu ya Faragha
  • Taarifa ya Mchapishaji

Haki miliki 2026: Hanns R. Neumann Stiftung

Sera ya Ufichuaji/Upigaji Filimbi

Rudi

1. Dhumuni

Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) inatarajia kila mtu anayefanya kazi kwa au na shirika kufuata viwango vya juu vya maadili. Malengo ya Sera hii ya Ufichuaji ni kuwahimiza wafanyakazi, washirika, wanufaika na washikadau wengine pamoja na wahusika wengine kuripoti maswala yenye mashaka kuhusu tabia isiyofaa au isiyo halali, bila kuogopa kulipiziwa kisasi au adhabu.

2. Upeo

Sera hii inatumika kwa wafanyakazi wote, wanakandarasi, washirika, washauri, wafanyakazi wa mafunzo, wafanyakazi wa kujitolea, na wengine wanaohusika na HRNS.

Pia inatumika kwa matawi yote na washirika wa HRNS. Hata hivyo, wanaweza kuchagua kutumia sera zao wenyewe mradi tu wanafuata kanuni/sheria katika sera hii kama kiwango cha chini zaidi.

3. Nini maana ya Ufichuaji/upigaji filimbi?

Ufichuaji au upigaji filimbi ni kuripoti utovu wa nidhamu unaoshukiwa, ukiukaji wa maadili, ukiukaji wa sera za kampuni, vitendo visivyo halali au kushindwa kutii majukumu ya kisheria. Hii inaweza kujumuisha, lakini sio tu kwa hizi:

  • Makosa ya jinai (k.m., udanganyifu, rushwa)
  • Ukiukaji wa majukumu ya kisheria au udhibiti
  • Hatari za kiafya na usalama
  • Uharibifu wa mazingira
  • Matumizi mabaya ya rasilimali za kampuni
  • Ubaguzi, unyanyasaji, au uonevu

4. Utaratibu wa Kuripoti

Maswala yenye mashaka yanatakiwa kuripotiwa haraka iwezekanavyo kupitia mojawapo ya njia zifuatazo:

  • Kupitia tovuti ya HRNS na fomu ya taarifa: Ripoti zilizowasilishwa kupitia fomu kwenye tovuti ya HRNS zinaelekezwa kwa Afisa wa Uzingatiaji wa HRNS au kwa mjumbe wetu wa nje wa malalamiko, kulingana na unavyotaka kuelekeza ripoti. Ripoti zinaweza kuwasilishwa kwa kuacha jina na/au maelezo ya mawasiliano, lakini pia kwa njia isiyojulikana.
  • Kwa kuwasiliana na mwangalizi wa nje:
    Dkt. Philipp Engelhoven
    Barua pepe: whistleblower.hrns@esche.de
    Anwani: Am Sandtorkai 44, 20457 Hamburg, Ujerumani
    Simu: +49 40 36805 119
  • Kwa kutuma barua pepe kwa Afisa Uzingatiaji wa HRNS:
    complianceoffice@hrnstiftung.org
  • Ikiwa wasiwasi wako ni kuhusu Afisa Uzingatiaji, tafadhali wasiliana na mwangalizi wa nje au Mkurugenzi Mkuu wa HRNS:
    Mkurugenzi Mtendaji Jens Sorgenfrei
    Barua pepe: managing.director@hrnstiftung.org
    Anwani: Hanns R. Neumann Stiftung, Am Sandtorpark 4, 20457 Hamburg, Germany
    Simu: +49 40 808112 406

Aidha, watoa taarifa wako huru kuwasiliana na ofisi za ripoti za nje kupitia wakala wa serikali. Mtu anayeripoti ukiukaji ana uhuru wa kuchagua ofisi ya kuripoti. Katika hali ambapo hatua madhubuti za ndani zinaweza kuchukuliwa dhidi ya ukiukaji wa kikanuni/kisheria unaowezekana na hakuna hofu ya kulipiziwa kisasi, kuripoti kupitia ofisi ya ndani ya kuwasilishia ripoti kunapendekezwa.

5. Usiri na Kutokujulikana

Ripoti zote zitashughulikiwa kwa usiri. Watoa taarifa wanaweza kuchagua kutokujulikana, ingawa hii inaweza kuzuia uwezekano wa uchunguzi kamili.

Kwa kuwasiliana na Afisa wa Uzingatiaji bila kujulikana, ripoti inaweza kuwasilishwa kupitia tovuti ya HRNS kwa kutumia fomu ya kuripoti na kuacha sehemu za hiari, yaani, jina, anwani ya barua pepe, tupu au kutumia akaunti ya barua pepe taka, k.m., trash-mail.com.

Kwa kuwasiliana na mwangalizi wa nje au Afisa Uzingatiaji bila kujulikana jina lako kupitia barua pepe au barua, unaweza kuomba utambulisho wako ubakie siri huku ukiendelea kuweka laini ya mawasiliano wazi. Afisa Uzingatiaji na mchunguzi wa nje ataheshimu matakwa yako ya usiri.

6. Ushughulikiaji wa maswala yenye mashaka yaliyolipotiwa

Mapokezi ya kila jambo lililoripotiwa litakubaliwa/idhinishwa kuwa limepokelewa ndani ya siku tano za kazi na mtu ambaye ripoti imeelekezwa kwake, lakini ikiwa tu utambulisho wa mtu aliyeripoti utafichuliwa au anwani ya urejeshaji majibu imetolewa.

Ripoti zote zitachunguzwa mara moja; hatua stahiki za urekebishaji zitachukuliwa iwapo itathibitishwa na uchunguzi.

7. Ulinzi dhidi ya kulipiza kisasi

HRNS inakataza kulipiza kisasi kwa mtu yeyote anayeibua maswala yenye mashaka kwa nia njema. Aina yoyote ya kulipiza kisasi itachukuliwa kama kosa kubwa la kinidhamu na inaweza kusababisha kusitishwa kwa ajira au ushirikiano.

8. Uchunguzi

Maswala yote yenye mashaka yaliyoripotiwa yatachunguzwa mara moja, kwa kina na bila upendeleo na mtu ambaye ripoti hiyo itakuwa imeelekezwa (Afisa Uzingatiaji, mwangalizi wa nje au Wakurugenzi Watendaji). Mtoa taarifa anaweza kuulizwa taarifa zaidi wakati wa uchunguzi ikiwa maelezo ya mawasiliano yalitolewa.

Ikiwa ripoti inahusiana na tuhuma ya utovu wa nidhamu/ukiukaji wa kanuni n.k. ya Afisa Uzingatiaji, jukumu la kuanzisha na kusimamia uchunguzi litakuwa moja kwa moja kwa Wakurugenzi Watendaji au mwangalizi wa nje aliyeteuliwa. Katika hali kama hizi, Afisa Uzingatiaji hatakuwa na jukumu katika mchakato wa uchunguzi. Menejimenti inaweza kushirikisha vyama huru vya nje ili kuhakikisha uchunguzi wa haki na usio na upendeleo.

9. Utunzaji wa kumbukumbu

HRNS itahifadhi ripoti zote na uchunguzi wote kwa usalama ndani ya miaka kumi.

10. Uhakiki wa Sera

Sera hii itafanyiwa uhakiki mara kwa mara na kusasishwa inapohitajika ili kuendelea kuwa na ufanisi na kulingana na mahitaji ya kisheria.

11. Mawasiliano

Afisa Uzingatiaji: Marion Schenk
Barua pepe: complianceoffice@hrnstiftung.org
Simu: +49-40-808112 419
Anwani: Am Sandtorpark 4, 20457 Hamburg, Germany

Hanns R. Neumann Stiftung, Julai 2025